Moja ya madereva akizungumza kwa niaba ya madereva wenzake walipofika kituo cha Polisi Osterbay

15 Oct . 2024

Wakili Peter madeleka akizungumza na wananchi mbele ya mhakama hii leo

15 Oct . 2024

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo

15 Oct . 2024

Kuelekea dabi ya Kariakoo Oktoba 19, 2024 Beki kisiki wa timu Yanga Ibrahimu Abdullah Hamad maarufu kama Bacca amemtumia salamu Mshambuliaji wa timu ya Simba Lionel Ateba kwa kumwambia wataonana uwanjani tarehe 19. Ateba wiki iliyopita alizungumza kwenye siku ya Vyombo vya Habari kwa Timu za Ligi kuu Tanzania bara kwamba haoni Mlinzi wa kumzuia kufunga siku ya dabi kutoka kwenye kikosi cha Wapinzani wao siku hiyo kikosi cha Yanga kinachonolewa na Mwalimu Miguel Gamondi.

15 Oct . 2024

Daniel Maldini ameweka rekodi ya kuwa Mwanaukoo wa tatu kutoka Familia ya Wacheza Soka nchini Italia baada ya jana Oktoba 14, 2024 kwenye mchezo wa ligi ya Mataifa ya Ulaya dhidi ya timu ya Taifa ya Israel Daniel amefuata nyayo za Babu yake Cesare Maldini na Baba yake Paulo Maldini wote kuitumikia The Azzurri kwa vizazi vitatu tofauti.Cesare alianza kuitumikia Italia 1960,Paulo 1988 na Daniel 2024.

15 Oct . 2024

Picha ya Alikiba na Diamond Platnumz wakiwa na dada zao

15 Oct . 2024

Timu ya Taifa ya Nigeria imepanga kugomea mchezo wa kufuzu AFCON 2025 Ugenini dhidi ya timu ya Libya. Kikosi cha Super Eagles kimeachwa uwanja wa Ndege kwa masaa 12 pasipo chakula wala maji ya kunywa, Wachezaji wamelazwa kwenye mabenchi ya Abiria huku mageti yakiwa yamefungwa na kutoa ugumu kwa timu ya Nigeria kuondoka uwanjani hapo.

14 Oct . 2024

Lamine Yamal amewastua Viongozi pamoja na Mashabiki wa Barcelona kuelekea mchezo wa La Liga dhidi ya Mahasimu Wao Wakubwa Real Madrid (El Clasico). Nyota huyo mwenye umri wa miaka 17 alitolewa nje ya Uwanja akiwa anachechemea kwenye mchezo dhidi ya Denmark muendelezo wa mechi za mashindano ya Mataifa Ulaya.

14 Oct . 2024

Mwanariadha wa Kenya mwenye umri wa miaka 30 Ruth Chepngetich ameweka rekodi mpya Chicago Marathon alitumia masaa mawili na dakika 9 na sekunde 57 na kuvunja rekodi iliyowekwa na Assefa mwaka 2023 ambaye alikimbia mbio ndefu kwa masaa mawili dakika 53 na sekunde 53. Chepngetich pia amewahi kushinda ubingwa wa Dunia mwaka 2019.

14 Oct . 2024