Beki wa Simba Che Malone Fondo amezungumzia mchezo wa dabi Oktoba 19, 2024 dhidi ya Yanga kwa kusema Wapinzani Wao wanaubora maeneo mengi ndani ya uwanja hivyo kufanya mechi baina yao kutokua rahisi, Che Malone ni mmoja wa Wachezaji wa kutumainiwa kwenye kikosi cha Wekundu wa Msimbazi anafahamu umuhimu wa kushinda mchezo huo kwani wakipoteza watakua wamefungwa kwenye mechi nne mfululizo dhidi ya Yanga
Jurgen Klopp mwenye umri wa miaka 57 amekubali kurejea kwenye soka lakini kwa kubadili majukumu yake ambapo kocha huyo wa zamani wa vilabu vya Mainz 05,Borrusia Dortmund na Liverpool ataanza kutekeleza majuku yake mapya Januari 1, 2025
Stars itaondoka majira ya saa 7 usiku leo kwenda Congo DRC kukabiliana na timu ya Congo DRC kwenye mchezo wa kufuzu AFCON 2025 itakayofanyika nchini Morocco Samata ataiongoza Stars huku Congo DRC ikimkosa mshambuliaji wa Brentford ya England Yoane Wissa
Ten Hag amejiunga United 2022 na kuiongoza timu hiyo kutwa kombe la ligi 2023, FA 2024 kocha huyo raia wa Uholanzi alisaini mkataba wa kubaki kwa Mashetani Wekundu kwa mwaka mmoja zaidi mwezi Juni 2024
kikosi cha Yanga kimepangwa kundi A makundi kombe la Klabu bingwa barani Afrika ambapo kwenye kundi hili zipo pia timu za Al Hilal ya Sudani, TP Mazembe kutoka Congo DRC na Mc Algers ya Algeria
Simba imepangwa kundi A kombe la shirikisho Afrika sambamba na CS Sfaxien ya Tunisia na CS Constantine ya nchini Algeria
