Alhamisi , 26th Sep , 2024

Aliyewahi kuwa mchezaji bora wa Ligi ya mpira wa kikapu ya Marekani NBA Derrick Rose ametangaza kustaafu kucheza mchezo wa kikapu akiwa na umri wa miaka 35, baada ya kucheza NBA kwa muda wa miaka 16.

Derrick Rose alikuwa MVP wa NBA mwaka 2011 akiwa na timu ya Chicago Bulls. Pia amecheza katika timu za New York Knicks, Cleveland Cavaliers, Minnesota Timberwolves, Detroit Pistons na Memphis Grizzlies. Alichaguliwa mara 3 kuwa kwenye kikosi cha NBA All Stars mara 3.

Ametangza kustaafu kucheza mpira wa kikapu kupitia mtandano wa kijamii wa instagram, lakini pia ameweka wazi ameutumikia mchezo wa mpira wa kikapu kwa miaka mingi sasa ni wakati wa kuwa na familia yake.