COSTECH yaagiza tafiti za kuchochea maendeleo
Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia COSTECH imewataka wasomi watafiti nchini kufanya tafiti za jinsi teknolojia inavyoweza kutumika katika kupunguza umaskini hususani jinsi ukuaji wa uchumi unavyoweza kuwa na maana katika pato la mtu mmoja mmoja.

