
Kocha mkuu wa Klabu ya Yanga Miguel Gamondi amesema ratiba ya Ligi Kuu ni ngumu kutokana na ukaribu wa michezo. Gamondi ameeleza hayo wakati mkutano na Waandishi wa habari kuelekea mchezo dhidi ya Coastal Unioni hapo kesho Oktoba 26 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

Kevin Durant amefunga kwenye dakika za nyongeza na kuipa ushindi timu yake ya Phoenix Suns wa Vikapu 116 dhidi ya vikapu 113 vya Los Angeles Clippers usiku wa Oktoba 23, mchezo uliochezwa uwanja wa Intuit Dome.

Kocha wa Liverpool ya Uingereza Arne Slot raia wa Uholanzi ameweka rekodi ya Kuwa Mkufunzi wa kwanza kushinda michezo 11 kati ya 12 iliyocheza mwanzoni mwa msimu na kuweke rekodi ya klabu hiyo

Klabu ya Namungo ya Ruangwa mkoani Lindi imemtangaza Juma Mgunda kuwa Kocha wao mkuu kuchukua nafasi ya Mwinyi Zahera ambaye amepangiwa majukumu mengine ndani ya klabu hiyo

Mfungaji bora wa muda wote wa NBA LeBron James usku wa jana Oktoba 22, 2024 aliweka rekodi nyingine kwenye ligi ya kikapu Marekani maarufu NBA. King aliweka rekodi ya kuchangia uwanja na mwanawe LeBron ‘Bronny’ James Jr mwenye umri wa miaka 20 kwenye mchezo uliozikutanisha LA Lakers dhidi ya Minnesota TimberWolves waliposhinda vikapu 110 kwa vikapu 103.

Nyota wa Real Madrid ya Hispania Vinicius Junior usiku wa jana Oktoba 22, 2024 aliushangaza ulimwengu wa Soka baada ya kuonyesha kiwango bora kwenye mchezo wa ligi ya Mabingwa barani Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund uwanja wa Santiago Bernabeu. Vini alifunga magoli matatu na kuiongoza Madrid kupata ushindi wa goli 5-2.

Klabu ya Coastal Union ya Tanga imemtangaza Juma Mwambusi kuwa kocha mkuu wa timu hiyo baada ya kumfuta kazi aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo David Ouma raia wa Kenya mwezi Agosti 2024. Kikosi hiko cha Wagosi wa Kaya kilikuwa chini ya Joseph Lazarao ambaye alikaimu kwa muda kipindi ambacho timu hiyo ilipokuwa inatafuta Mwalimu Mkuu.

Nahodha wa zamani wa Uruguay na Mchezaji wa klabu ya Manchester United ya England atashiriki mashindano ya Tennis yatakayofanyika Uruguay Montevideo. Forlan ana umri wa miaka 45 atashirikiana na Federico Coria kwenye michezo ya wawili kwa wawili.

Aishi Manula mara ya mwisho kuitumikia timu ya taifa ya Tanzania ilikua mwezi Machi 2024.Kumekua na mjadala mkubwa kwa Wapenzi na Wadau wa soka nchini Tanzania kuhusiana na nafasi ya Golikipa huyo wa timu ya Simba kwenye kikosi cha Stars. Manula hana Wakati mzuri kwenye klabu yake ya Simba ameondolewa kwenye nafasi yake ya kuwa golikipa namba moja baada ya kuumia kwa muda mrefu na aliporejea uwanjani kwenye mchezo wa Dabi ya Kariakoo alifanya makosa yaliyochangia kupoteza mchezo kwa goli 5-1.

Wachezaji wa timu za taifa za Wanawake zaidi ya 100 wameliandikia barua ya wazi Shirikisho la mpira Duniani FIFA kulitaka kuvunja mkataba wake wa udhamini na kampuni ya mafuta ya Saudi Arabia ya Aramco. Sababu kubwa zilizotajwa na Wachezaji hao ni kutokana na uharibifu wa Mazingira unaofanywa na kampuni hiyo ya uchimbaji wa mafuta, pamoja na uvunjwaji wa Haki za Binadamu nchini SaudI Arabia. Uwepo wa tamaduni ambazo zinamkandamiza Mwanamke nchini humo inatizamwa kama sababu kubwa zaidi ya Wachezaji wa timu za Wanawake kugomea mkataba huo wa udhamini. Aramco imesaini mkataba na FIFA utakaofika tamati mwaka 2027 ambapo kampuni hiyo itadhamini kombe la Dunia la Wanaume 2026 na Wanawake 2027.

Barani Ulaya kwa sasa Wachezaji Wanaongoza kwa ufungaji wa magoli kwenye ligi kuu Tano kubwa ni Washambuliaji wa kati. Mabadiliko ya Sayansi ya mpira wa miguu imepelekea kupoteza baadhi ya Wachezaji ambao walisifika kwa kutimiza majukumu yao yaliyokuwa yanawaweka ndani ya uwanja.Mabadiliko wa kiucheza na mifumo mipya kwenye mpira wa miguu imepelekea kuibuka kwa Wachezaji wa pembeni yao Mawinga kutumika kama Washambuliaji wa kati na kumfanya namba Tisa ili aweze kucheza awe na sifa ya kuchezesha wengine kama kiungo wa kutokea juu yaani inside Forward. Harry Kane, Karim Benzema na Robert Firmino ni mfano sahihi wa Washambuliaji wa kati wenye uwezo wa kuchezesha wengine ndani ya uwanja.

Moussa Camara Golikipa mpya raia wa Guinea alibeba matumaini makubwa ya Wana Msimbazi kwa kupata Mlinda Mlango ambaye anauwezo wa kucheza mpira kwa miguu yake. Katika michezo miwili mfululizo nyota huyo amefanya makosa ambaye yameigharimu klabu ya Simba alama 5 ambazo zinaweza kuwa alama muhimu kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu ambao timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi Karikaoo imeutafuta kwa misimu mitatu mfululizo bila mafanikio.

Harry Kane Mshambuliaji wa Bayern Munich jana alifunga goli tatu hat-trick dhidi ya Stuttgat na kufikisha idadi ya hat-trick Sita tangu ajiunge na Bavarians kutokea Tottenham Hotspurs ya Uingereza. Kane anashikilia rekodi ya kuwa Mchezaji mwenye asili ya Uingereza aliyefunga goli nyingi zaidi kwenye ligi kuu nchini Ujerumani mbele ya Kevin Keegan, Jude Bellingham na Tony Woodcock.

Yanga SC imeshinda mchezo wa Dabi jana kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Wapinzani wao wa jadi timu ya Simba. Yanga ilicheza kwa heshima kubwa kwa kufahamu Simba SC ingekuja kwa nia ya kushambulia kuanzia dakika ya kwanza mchezo kutokana na matokeo ya nyuma dhidi ya Wapinzani wao. Ubora wa Yanga ni mkubwa sana na hii inajidhihirisha kutokana na kuchukua ubingwa mara tatu mfululizo huku ikiwa inatafuta ubingwa wake wa nne kama itafanikiwa kuutetea ubingwa wa ligi msimu huu wa 2024-2025. Ushidni wa jana ni wa nne mfululizo mbele ya Watani wao wa jadi na majirani zao mitaa ya Karikoo Simba SC, Simba imebadilika chini ya Kocha Fadlu Davies lakini bado haijawa timu kamili ambayo inayoweza kubishana na Yanga kutokana na uzoefu wa Yanga kucheza akitimu na utofauti wa madaraja ya mchezaji mmojammoja.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akipambana na vijana wa Shule ya Sekondari Kijitonyama.