Yanga SC imeshinda mchezo wa Dabi jana kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Wapinzani wao wa jadi timu ya Simba. Yanga ilicheza kwa heshima kubwa kwa kufahamu Simba SC ingekuja kwa nia ya kushambulia kuanzia dakika ya kwanza mchezo kutokana na matokeo ya nyuma dhidi ya Wapinzani wao. Ubora wa Yanga ni mkubwa sana na hii inajidhihirisha kutokana na kuchukua ubingwa mara tatu mfululizo huku ikiwa inatafuta ubingwa wake wa nne kama itafanikiwa kuutetea ubingwa wa ligi msimu huu wa 2024-2025. Ushidni wa jana ni wa nne mfululizo mbele ya Watani wao wa jadi na majirani zao mitaa ya Karikoo Simba SC, Simba imebadilika chini ya Kocha Fadlu Davies lakini bado haijawa timu kamili ambayo inayoweza kubishana na Yanga kutokana na uzoefu wa Yanga kucheza akitimu na utofauti wa madaraja ya mchezaji mmojammoja.

20 Oct . 2024

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akipambana na vijana wa Shule ya Sekondari Kijitonyama.

18 Oct . 2024

Bodi ya ligi kuu Tanzania bara imemtangaza Ramadhani Kayoko kusimamia sheria kumi na saba kwenye mchezo wa Dabi ya Kariakoo mchezo unaozikutanisha timu za Simba SC dhidi ya Yanga SC katika uwanja wa Benjamini Mkapa. Mchezo huo mkubwa nchini Tanzania na Afrika ya Masharaiki utachezwa kesho Jumamosi saa 11:00 jioni. Watakaomsaidia Kayoko ni Mohamed Mkono kutoka Tanga na Kassim Mpanga huku Tatu Malogo atakuWa Muamuzi wa mezani.

18 Oct . 2024

Trent- Alexander Arnold amegomea mkataba mpya wa kusalia kikosi cha Liverpool na kuamsha presha kwa Mabosi wa klabu hiyo juu ya mustabali wa mchezaji huyo ndani ya timu hiyo. Taarifa zinazowastua zaidi Uongozi wa Majogoo wa Jiji ni kuhusiana na jina la nyota huyo kuwepo kwenye listi ya Wachezaji wanaohitajika kwenye kikosi cha Real Madrid ya Hispania dirisha kubwa usajli mwezi Julai 2025.
Mkataba wa Trent ndani ya Liverool unatamatika mwishoni mwa msimu wa 2024-2025.

17 Oct . 2024

Fred Felix Minziro amejiunga na timu ya Pamba ya Jijini Mwanza baada ya timu hiyo kumfuta kazi Goran Kopunovic. Pamba imeshacheza michezo saba ya ligi kuu Tanzani bara msimu huu wa 2024-2025 mpaka sasa, imetoka sare michezo minne na kupoteza michezo mitatu na inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi ikiwa imejikusanyia alama 4.

17 Oct . 2024

Kocha wa zamani wa klabu ya Simba amesaini mkata wa kuitumikia timu ya Al Ahly Tripoli ya nchini Libya. Didie Gomes Da Rosa alikuwa akifundisha timu ya taifa ya Botswana kabla ya kujiuzulu nafasi yake na kutangazwa kwenye klabu hiyo ya Libya kuwa Kocha wao mkuu. Gomes raia wa Ufaransa alishinda taji la ligi kuu Tanzania bara, kombe la shirikisho Tanzania ( FA ) na aliiwezesha klabu ya Wekundu wa Msimbazi kucheza hatua ya robo fainali kombe la klabu bingwa Afrika msimu wa 2021.

17 Oct . 2024

Thomas Tuchel kocha wa zamani wa Chelsea ya England amesaini mkataba wa miezi 18 kuiongoza timu ya taifa ya England. Kikosi hicho mabingwa wa kombe la Dunia mwaka 1966 kilikua chini ya Kocha wa muda Lee Carsley baada ya aliyekua Mkufunzi mkuu wa timu hiyo Gareth Southgate kujiuzulu mwezi Julai 2024. Tuchel anakuwa Mwalimu wa tatu ambaye si raia wa Uingereza kuiongoza England baada ya Sven- Goran Eriksson na Fabio Capello. Mjerumani huyo aliyewahi kushinda tuzo ya Kocha bora Ulaya na Dunia mwaka 2021 atasaidiwa na Antony Barry aliyefanya naye kazi Chelsea na Bayern Munich.

16 Oct . 2024

Nyota wa zamani wa klabu ya Manchester United ameujia juu Uongozi wa Manchester United baada ya Mabosi wa klabu hiyo kumuondoa Sir Alex Ferguson kwenye nafasi yake ya Ubalozi wa Mashetani Wekundu wa Jiji la Manchester. Ferguson Kocha mwenye mafanikio zaidi katika historia ya Mameneja wa Kingereza, aliiongoza Man U kushinda makombe 13 ya ligi kuu Uingereza, Kombe la ligi ya mabingwa barani Ulaya mara mbili na Kombe la klabu bingwa Dunia msimu wa 2007-2008. Cantona alikuwa Mchezaji muhimu alitoa mchango mkubwa kwenye klabu ya Manchester United alishinda makombe ya ligi EPL mara 4 katika miaka 5.

16 Oct . 2024

Kuelekea dabi ya Kariakoo Oktoba 19, 2024 Beki kisiki wa timu Yanga Ibrahimu Abdullah Hamad maarufu kama Bacca amemtumia salamu Mshambuliaji wa timu ya Simba Lionel Ateba kwa kumwambia wataonana uwanjani tarehe 19. Ateba wiki iliyopita alizungumza kwenye siku ya Vyombo vya Habari kwa Timu za Ligi kuu Tanzania bara kwamba haoni Mlinzi wa kumzuia kufunga siku ya dabi kutoka kwenye kikosi cha Wapinzani wao siku hiyo kikosi cha Yanga kinachonolewa na Mwalimu Miguel Gamondi.

15 Oct . 2024

Daniel Maldini ameweka rekodi ya kuwa Mwanaukoo wa tatu kutoka Familia ya Wacheza Soka nchini Italia baada ya jana Oktoba 14, 2024 kwenye mchezo wa ligi ya Mataifa ya Ulaya dhidi ya timu ya Taifa ya Israel Daniel amefuata nyayo za Babu yake Cesare Maldini na Baba yake Paulo Maldini wote kuitumikia The Azzurri kwa vizazi vitatu tofauti.Cesare alianza kuitumikia Italia 1960,Paulo 1988 na Daniel 2024.

15 Oct . 2024

Timu ya Taifa ya Nigeria imepanga kugomea mchezo wa kufuzu AFCON 2025 Ugenini dhidi ya timu ya Libya. Kikosi cha Super Eagles kimeachwa uwanja wa Ndege kwa masaa 12 pasipo chakula wala maji ya kunywa, Wachezaji wamelazwa kwenye mabenchi ya Abiria huku mageti yakiwa yamefungwa na kutoa ugumu kwa timu ya Nigeria kuondoka uwanjani hapo.

14 Oct . 2024

Lamine Yamal amewastua Viongozi pamoja na Mashabiki wa Barcelona kuelekea mchezo wa La Liga dhidi ya Mahasimu Wao Wakubwa Real Madrid (El Clasico). Nyota huyo mwenye umri wa miaka 17 alitolewa nje ya Uwanja akiwa anachechemea kwenye mchezo dhidi ya Denmark muendelezo wa mechi za mashindano ya Mataifa Ulaya.

14 Oct . 2024

Mwanariadha wa Kenya mwenye umri wa miaka 30 Ruth Chepngetich ameweka rekodi mpya Chicago Marathon alitumia masaa mawili na dakika 9 na sekunde 57 na kuvunja rekodi iliyowekwa na Assefa mwaka 2023 ambaye alikimbia mbio ndefu kwa masaa mawili dakika 53 na sekunde 53. Chepngetich pia amewahi kushinda ubingwa wa Dunia mwaka 2019.

14 Oct . 2024

Bondia wa Australia amefanikiwa kutetea ubingwa wake wa WBC uzito wa Unyoya baada ya kupata ushindi wa pointi kutoka kwa Majaji walioshuhudia pambano hilo. Pambano la kwanza la ubingwa kwa uapande wa Wanawake kufanyika nchini Saudi Arabia limetizamwa kama ni hatua chanya kwa Taifa hilo kwenye michezo kwa upande wa Wanawake na tunaweza kuanza kushuhudia Mabondia Wakike kutoka Saudi Arabia wakipambana ulingoni.

13 Oct . 2024

Nahodha wa Ureno Criastiano Ronaldo amefunga goli lake la 133 akiwa na jezi ya timu ya Taifa lake kwenye mchezo waliocheza ugenini dhidi ya Poland siku ya jana Oktoba 12, 2024, kumfanya aendelee kuiweka vizuri rekodi yake ya kuwa Mchezaji aliyefunga goli nyingi kwenye michezo rasmi ya kimataifa kwa upande wa Wanaume. Kwenye ushindi dhidi ya Poland Ronaldo amefikisha goli la 903 tangu aanze kucheza soka.

13 Oct . 2024