Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kenya yasitisha safari za Uingereza

Tuesday , 6th Apr , 2021

Shirika la Ndege la Kenya Airways limesitisha safari zake kuelekea Uingereza kufuatia mzozo wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili, hivyo watu wanaotaka kusafiri kwenye mataifa hayo wametakiwa kufikia tarehe tisa mwezi huu, kabla ya hatua hiyo kuanza kutekelezwa.

Wizara ya mambo ya nje ya wingereza ilikuwa ya kwanza kutoa ilani kwa raia wanaosafiri wingereza kutoka Kenya na mataifa mengine Afrika, ilani iliyotolewa na kuwataka wasafiri na ndege zote zinazotoka mataifa hayo kusitisha safari zake, ikitaja maambukizi ya virusi vya corona kuwa chanzo cha hatua hiyo.

Kenya kwa upande wake ikijibu Uingereza, ilisema kuwa hatua hiyo imaonyesha mapendeleo na ubaguzi, kwani taifa hili linaendelea kuchukuwa tahadhari zote kwa mujibu wa shirika la afya ulimwenguni, hivyo haikustahili kuwa kwenye orodha ya mataifa yanayozuiliwa kuenda wingereza.

kwa taarifa ya Wizara ya mambo ya Nje ya Kenya kwa vyombo vya habari, imeijibu uingereza kwa kuwawekea vikwazo raia wa uingereza wanaosafiri kuingia Kenya, au ndege zozote zinazo tokea huko Uingereza ambapo ni sharti raia wake wawekwe karantini ya lazima kwa siku kumi nane, kinyume na ilivyokuwa awali na watahitajika kulipia karantini hiyo pamoja na kuhitajika kupimwa corona mara mbili.

Kenya inaeleza kuwa hatua ya Uingereza kwa mataifa hayo ya afrika yaliyotajwa kwenye orodha hiyo inaonyesha ubaguzi na maendeleo, ikisema kuwa hii itavuruga uhusiani mwema kati ya mataifa hayo na uingereza kibiashara, utalii na sekta zingine muhimu.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja