Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa
Waziri Mchengerwa ametishia kuwaondoa kwenye nafasi zao viongozi wote wanaohusika kukwamisha watumishi kupanda madaraja katika ngazi mbalimbali huku akisisitiza jambo la watumishi kupandishwa madaraja kuwa ndio kipaumbele chake.
Mchengerwa ameyasema hayo wakati akifungua maadhimisho ya 51 ya siku ya Wauguzi yanayofanyika Kitaifa mkoani Tanga ambapo katika hotuba yake Rais wa chama cha wauguzi Tanzania Alexander Baluhya alisema mbele ya Waziri Mchengerwa kuwa jambo hilo limekuwa kilio chao cha muda mrefu sasa hususani kwa watumishi waliopo muda mrefu kazini.