Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wakulima wa mbogamboga walia mbegu bora za kusia

Wednesday , 16th Sep , 2020

Wafanyabiashara na wakulima wa kilimo cha mboga mboga jijini Dar es salaam wamesema changamoto kubwa inayowakabili ni upatikanaji wa mbegu bora pamoja na mbolea ya samadi wanayotumia.

Katika maeneo mbalimbali ya jiji pamekuwepo na watu wakijihusisha na biashara ya mboga za majani wengi wakilipa jina la kilimo cha Mjini ambapo hapa EATV imefika katika maeneo yao ya uzalishaji ili kuuona uhalisia ulivyo kwa Sasa katika biashara hiyo ambayo huchangia kwa kasi katika kuboresha afya ya mwili.

"Kusema ukweli mbegu ni tatizo pamoja na mbolea maana sisi tunaumia mbolea ya Samadi sio zile za dukani kwa iyo Kuna muda wafugaji wa kuku nao wanakuwa na uhaba hivyo tunapata shida,pia Niwaombe maafisa ugani watoke ofisini wawasaidie wakulima kujua kipi kinatakiwa Ili kuongeza mavuno" Mary Kibasa Mkulima wa mboga mboga.

Akizungumzia kilimo hicho bw Seif Mohamed wakati akifanya mahojiano amesema eneo hilo ni hifadhi ya barabara akiiomba serikali kuwapatia maeneo ambayo wanaweza kufanya kilimo hicho cha Mjini kwa kiasi kikubwa zaidi kwa kuwa hunufaisha watu wengi wakiwemo wauzaji wa mbolea,mbegu na mboga mboga kwa ujumla.

"Hapa tulipo tunalima kwa zaidi ya miaka 20 sasa lakini ni kwenye hifadhi ya barabara kwaiyo tungeomba serikali kama kuna maeneo ambayo wanahisi hajaendelezwa wangetupatia sisi tunafanya kilimo cha mjini kama hiki"alisema Seif Mohamed Mkulima wa mbogamboga.

Wamesema katika eneo hilo wao hutumia maji safi ya bomba kumwagilia mboga mboga hizo tofauti na watu wengi ambao wamekuwa wakisambaza uvumi kuwa walimaji wa kilimo cha mjini hutumia maji yasiyo salama kumwagilia wakiwasisitiza tuu maafisa ugani kutoka manispaa kuzidi kuhamasisha kilimo cha mjini.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja