Nyota wa Golden State Warriors Stephen Curry amepata majeraha timu yake ikipoteza dhidi ya Los Angeles Clippers kwa alama 112-104. Curry alipata majeraha kwenye mchezo wa ligi ya kikapu nchini Marekani maarufu NBA dhidi ya Clippers mchezo uliochezwa jana Jumapili Oktoba 27, uwanja wa Chase Center.