Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Lowassa, Sumaye sababu ya Kubenea kubaki CHADEMA

Wednesday , 6th Dec , 2017

Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amesema kwamba hawezi kuhama CHADEMA na kwenda CCM wakati yeye alishughulika kuwashawishi baadhi ya watu kuhamia katika chama alichopo sasa hivi.

Kubenea amesema kwamba ana mchango mkubwa sana katika kumuingiza Lowassa pamoja na Sumaye CHADEMA hivyo angejiona  mwendawazimu kuwasaliti watu ambao walimuamini na kwenda kwenye Chama ambacho yeye aliwaondoa.

"Mimi ningetaka kuondoka CHADEMA, ningeondoka kwa dhamira yangu mwenyewe lakini siyo kwa kushawishiwa au kwa kufika bei. Bei yangu ni utu wangu. Mimi sina bei kabisa hata kama Ingetengwa bajeti nzima ya serikali isingeweza kuninunua. Kiufupi sina bei.  Nimejenga jina kwa miaka 15 pamoja na sifa nzuri za chama changu nili struggle kwa kupata nafasi ya kutunga sheria siwezi kuwasaliti watu wa ubungo na hata wale walionichangia sumni sumni" Kubenea.

Mh. Kubenea

Ameongeza kwamba "Naendaje CCM, wakati huo huo mimi nilishiriki kuwavuta CHADEMA Mawaziri Wakuu wawili Lowassa na Sumaye. Sasa kweli nawezaje kuhama chama na kuwaacha hao watu na wengine wengi tu kwa ajili ya kuhamia CCM nitakuwa sina akili. Uweli nimeumizwa na huo uzushi.

Mbali hayo Kubenea ameongeza kwamba  anashangaa Chama hicho kinachoitwa cha wanyonge (CCM) kimefukuza wafanyakazi wengi wanaodaiwa kutokuwa na vyeti lakini watu waliofukuzwa walitumikia nchi kwa miaka mingi na wamefukuzwa kazi bila hata kifuta jasho huku kukiwa na mtu ambaye anatumia jina lisilo lake na chama chake kinamkumbatia.

Amefafanua kuwa wakati mwingi alikuwa akitumia nafasoi na tashi wake katika kukosoa hivyo hajaona jipya ambalo CCM wanaweza kufanya kwani hata hicho kinachoitwa kupambana na rushwa wameshindwa na badala yake kimempandisha cheo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru na kuwa Mkuu wa Mkoa licha ya kutuhumiwa kwa rushwa na ushahidi ulionyesha

Pamoja na hayo kubenea ameweka wazi kwamba "Hakuna jambo ndani ya chamba changu ambacho kinaweza kunishawishi mimi kukihama
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja