Wazawa kushiriki uchumi wa mafuta na gesi - wizara
Moja ya mitambo inayotumika katika utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi katika kina cha bahari kuu.
Serikali ya Tanzania imesema itahakikisha katika sera ya mafuta na gesi inayokuja, wazawa katika maeneo yanakochimbwa mafuta na gesi wanapewa kipaumbele cha kwanza katika kuwawezesha kiuchumi.