Kuna muda nilishindwa kutabasamu - Chid Benz
Msanii wa Bongo Flava Chid Benz amesema kwamba akifikiria maisha ya nyuma anakumbuka kuna wakati alikosa kutabasamu kutokana na hali ya madawa ambayo ilikuwa ikimuandama ambayo anasema kwa sasa ameweza kuachana nayo.

