Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Rais Samia ni wa mfano kimataifa" - Dkt Mwigulu

Sunday , 4th Dec , 2022

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt Samia, amekuwa akipigiwa mfano na mashirika ya fedha ya kimataifa na nchi mbalimbali duniani kwa ubunifu mkubwa wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotokana na fedha za mkopo usiokuwa na riba wa Benki ya Dunia wa Tril 1.3.

Waziri wa Fedha na Mipano, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, akizungumza na wakazi wa Kata ya Kaselya,

Kwa ajili ya kukabiliana na athari za kiuchumi zinazotokana na changamoto ya UVIKO 19.

Hayo ameyabainisha baada ya wakazi wa Kata ya Kaselya, wilayani Iramba mkoani Singida, kuondokana na adha ya maji baada ya kukamilika kwa mradi wa maji wa Kaselya uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 770.

Wakazi hao wameishukuru serikali kwa kufanikisha na kukamilisha ujenzi wa mradi huo, wakati wa ziara ya Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba, alipotembelea na kukagua mradi huo ambao fedha zake zinatokana na mradi wa kukabiliana na athari za UVIKO 19.

"Tunakuomba utupelekee salamu nyingi kwa Rais Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kututatulia changamoto ya maji kafika Kata yetu, ametutua ndoo kichwani wanawake na wewe Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango na Mbunge wetu kwa jitihada zako za kufanikisha mradi huu na miradi mingine," walisema wakazi wa kata hiyo

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameahidi kumfikishia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pongezi za wananchi hao kwa jitihada zake za kuwaletea wananchi maendeleo kwa kasi kubwa.

Akiwa jimboni, Dkt. Nchemba ametembelea na kukagua ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa miundombinu ya madarasa  ya shule ya sekondari Ndulungu, kituo cha afya Mwandegembe, shule ya sekondari Mbelekese, kituo cha afya Urugu na kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika tarafa ya Ndago.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa