Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Vibonde' wa Yanga watua Dar kwa kishindo

Thursday , 16th Feb , 2017

Wapinzani wa Yanga katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika timu ya Ngaya kutoka Comoro wamewasili leo jijini Dar es Salaam tayari kabisa kwa mchezo wa marudiano utakaochezeshwa na waamuzi kutoka nchini Uganda.

Kikosi cha Ngaya kutoka Comoro kikiwasili hii leo Uwanja wa Ndege Jijini Dar es salaam

 Timu hiyo imewasili leo saa saba na nusu mchana kwa ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATC), huku ikiwa imeongozana na baadhi ya viongozi wake.

Mara baada ya kuwasili timu hiyo ilipokelewa na wananchi wa nchi hiyo wanaoishi hapa nchini hata hivyo viongozi wa timu hiyo hawakuwa tayari kuzungumza chochote na wanahabari badala yake walipiga picha ya pamoja na wachezaji na kisha kupanda kwenye magari na kuondoka. 

Kuelekea katika mchezo huo utakaopigwa Jumamosi hii katika dimba la Taifa, Kocha Msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi amesema, bado wanaangalia umuhimu wa dakika 90 za marudiano ili kuhakikisha wanapata ushindi wa nyumbani.

Akizungumza jijini Dar es salaam Kocha Mwambusi amesema, wanaamini kiwango cha wapinzani wao ni kizuri na bado watahitaji kupambana lakini kwa upande wao wamejipanga ili kuhakikisha wanapata ushindi utakaowapa nafasi ya kusonga mbele.

“Tunatambua umuhimu wa mchezo wetu wa marejeano ambao utafanyika siku ya Jumamosi, Ngaya siyo timu mbaya kwasababu hata ukiangalia dakika tuliyoanza kupata goli la kwanza inaonesha ni kiasi gani wamejipanga, kikubwa tunawaomba mashabiki wetu na wanamichezo wajitokeza kwa wingi kuipa sapoti timu yao,” alisema.

Katika mchezo wa Kwanza Yanga ilishinda mabao 5-1, hali inayoashiria ugumu kwa timu hiyo ya Comoro kuvuka katika hatua hiyo.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa