Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mufindi waibana serikali kuhusu barabara

Saturday , 6th Dec , 2014

Wananchi wa vijiji vya Igowole na Mufindi Kibaoni wilayani Mufindi wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya Nyololo Igowole hadi Mgololo yenye urefu wa kilomita 77.6

Wananchi wa vijiji vya Igowole na Mufindi Kibaoni wilayani Mufindi wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya Nyololo Igowole hadi Mgololo yenye urefu wa kilomita 77.6 kwani barabara hiyo ni muhimili kwa uchumi wa wilaya ya mufindi na taifa kwa ujumla kutokana na uwepo wa viwanda vikubwa kikiwemo kiwanda cha karatasi cha mgololo.

Wananchi hao wamesema hayo kwenye mikutano ya hadhara iliyofanywa na Naibu Waziri wa Ujenzi mhandisi Gerson Lwenge wakati alipotembelea kukagua barabara na kuongea na wananchi wa vijiji vinavyopitiwa na barabara hiyo ambapo wananchi hao wamemwambia Naibu Waziri huyo kuwa wamekuwa wakiahidiwa kujengewa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kwa muda mrefu sasa lakini utekelezaji wake umekuwa kitendawili.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi katika kijiji cha Kibaoni bwana Jacob Sanga amesema ahadi za serikali zisizoambatana na utekelezaji kujenga barabara  hiyo zinakweka chama hicho tawala katika wakati mgumu ambapo wao kama viongozi wamekosa majibu ya kuwapa wananchi wanapohoji utekelezwaji wa ahadi hiyo ya serikali.

Akijibu malalamiko hayo Naibu Waziri wa Ujenzi Gerson Lwenge amesema serikali imeshaanza hatua za ujenzi wa barabara hiyo kwa kufanya upembuzi yakinifu hivyo kuwatoa hofu wananchi hao na kwamba serikali ina thamini mchango unaotolewa viwanda vya chai, kahawa na karatasi vinavyotegemea barabara hiyo kwa ajili ya kusafirisha malighafi pamoja na bidhaa zinazotoka viwandani humo.

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari