Gerezani
Mahakama imeeleza kuwa mtuhumiwa alifanya kitendo hicho Februari 09, 2024 cha kumbaka mwanafunzi huyo kwa kumlaghai kwa kumapatia zawadi ya soda kisha kwenda nae shambani kwake na kumbaka.
Kesi ilisikilizwa na upande wa mashitaka ulileta mashahidi watano ambao walithibitisha kosa na mtuhumiwa alitiwa hatiani kwa mujibu wa sheria.
Mbele ya Mhe. Lefi Sizya SRM, Mahakama imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kubaka ili iwe fundisho kwa watu wengine.