Trent- Alexander Arnold amegomea mkataba mpya wa kusalia kikosi cha Liverpool na kuamsha presha kwa Mabosi wa klabu hiyo juu ya mustabali wa mchezaji huyo ndani ya timu hiyo. Taarifa zinazowastua zaidi Uongozi wa Majogoo wa Jiji ni kuhusiana na jina la nyota huyo kuwepo kwenye listi ya Wachezaji wanaohitajika kwenye kikosi cha Real Madrid ya Hispania dirisha kubwa usajli mwezi Julai 2025.
Mkataba wa Trent ndani ya Liverool unatamatika mwishoni mwa msimu wa 2024-2025.

17 Oct . 2024

Fred Felix Minziro amejiunga na timu ya Pamba ya Jijini Mwanza baada ya timu hiyo kumfuta kazi Goran Kopunovic. Pamba imeshacheza michezo saba ya ligi kuu Tanzani bara msimu huu wa 2024-2025 mpaka sasa, imetoka sare michezo minne na kupoteza michezo mitatu na inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi ikiwa imejikusanyia alama 4.

17 Oct . 2024