Wanazuoni waonesha wasiwasi kuhusu Zanzibar
Wanazuoni na Wachambuzi wa masuala ya siasa wameonyesha hali ya wasiwasi wa hali ya kisiasa visiwani Zanzibar baada ya Tume ya Uchaguzi visiwani humo kutaka uchaguzi urudiwe na kusema kuwa hali hiyo inaweza kusababisha mgogoro mkubwa visiwani humo.

