Jumapili , 23rd Mar , 2014

Msanii Young Killer ambaye amerudi kwa kasi katika chati za muziki na ngoma yake mpya ambayo inakwenda kwa jina “My Power” ambayo amemshirikisha Damiani Soul, amesema tangu afahamike na wengi kupitia muziki, amepoteza idadi kubwa ya marafiki.

Msanii Young Killer

Tofauti na wengi walivyotegemea, Young Killer amesema kuwa, Muziki umempunguzia marafiki, lakini pia rapa huyu akakiri kuwa muziki huu huu umemkutanisha na kumpatia nafasi ya kufahamiana na watu wengi.

Young Killer pia amezungumzia ukali wa ngoma zake ambapo amesema kuwa, yeye hutumia muda mrefu sana katika kuandika mashairi ya muziki wake, kitu ambacho kinafanya mashairi yake kukubalika kwa kiasi kikubwa kila kukicha na idadi kubwa ya watu.