Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watumishi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu waonywa

Alhamisi , 25th Aug , 2016

Naibu mwanasheria mkuu wa Serikali, Gerson Mdemu amewataka watumishi wanaofanya kazi kwenye ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali kufanyakazi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu ili kuifanya ofisi hiyo kuwa ya mfano mzuri wa kuigwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. George Mcheche Masaju .

Mdemu ametoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo ya uongozi ya kuwajengea uwezo mawakili na waendesha mashtaka wa serikali nchini yaliyofanyika katika ukumbi wa hazina mjini hapa.

Amesema watumishi hao ni lazima wafuate kanuni na maadili ya viongozi wa umma wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao ya kila siku ikiwa ni pamoja na kutunza siri na viapo vyao.

“Mafunzo hayo yakawe chachu ya kuwawezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali mnazokabiliana nazo katika kutekeleza majukumu yenu ya kila siku,” alisema Mdemu.

Naye Neema Mwanda ambaye ni wakili mfawidhi wa serikali kutoka Mkoani Kilimanjaro amesema kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni aina za uhalifu na watu wanaofanya uhalifu huo nchini.

Amesema kila kukicha nchini kuna aina mbalimbali za uhalifu unaotokea na kufanywa na watu tofauti tofauti hivyo kuleta changamoto kubwa kwao namna ya kukabiliana na kesi za aina hiyo.

Kwa upande wake wakili mfawidhi mkuu kutoka mkoani Mbeya Joseph Pande, amesema kuwa wana wajibu mkubwa wa kuwasimamia mawakili wa serikali katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku bila kupendelea mtu au kundi lolote.

Amesema ili mawakili na wanasheria wa serikali waweze kutekeleza majukumu yao ya kila siku ni lazima wafuate kanuni, sheria na utaratibu na miongozo iliyopo ili waweze kutenda haki katika kazi zao.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja