Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TRA yaiachia sukari iliyokuwa inashikiliwa Mbagala

Jumanne , 10th Mei , 2016

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imeachilia tani elfu 6,757 za sukari iliyokutwa kwenye maghala ya forodha huko Mbagala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam iliingizwa nchini kihalali kwa kufuata taratibu zote za uingizaji sukari nchini.

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipakodi wa TRA Bw. Richard Kayombo

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipakodi wa (TRA) Bw. Richard Kayombo, ameia embia EATV kuwa sukari hiyo iliingizwa nchini na kampuni ya Al-Naeem na ilikuwa ikisubiri vibali kutoka Bodi ya Sukari, Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na kukamilisha taratibu za kodi.

"Baada ya kupitia na kufanya ukaguzi wa kila hatua tumejiridhisha kuwa tani 6,757 za sukari tulizokuwa tunazishikilia katika maghala ya forodha huko Mbagala zimeingizwa nchini kwa kufuata taratibu zote na hivyo tumeona hakuna haja ya kuendelea kushikilia shehena hiyo," alisema Bw. Kayombo.

Kwa mujibu wa Bw. Kayombo, mmiliki wa shehena hiyo ameruhusiwa kuanza kuisambaza sukari hiyo katika mzunguko wake wa kibiashara na kwamba kuwepo kwake sokoni huenda kukasaidia kupunguza bei na makali ya upatikanaji wa sukari nchini. Aliongeza kuwa "Tuna imani kuwa baada ya shehena hii kuingizwa sokoni, uhaba wa sukari utapungua na bei yake itarejea kuwa ya kawaida,".

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Kampuni ya Al-Naeem Bw. Eddy Salim amesema baada ya ruhusa hiyo ya serikali, wamejipanga kuhakikisha sukari inasambazwa katika maduka yao yote huku wakihakikisha kuwa bei inabaki kuwa ya kawaida.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja