Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyumba zawafikisha Wahadzabe serikalini

Jumatano , 27th Sep , 2017

Wananchi jamii ya Wahadzabe wanaoishi kwa maisha ya asili ya kula nyama, asali  na matunda huku wakilala nyumba za nyasi  wameomba serikali kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF awamu ya tatu kuwajengea nyumba imara ili waache

maisha ya kuhamahama wakati wa mvua.

Mwenyekiti jamii ya Wahadzabe kutoka kijiji cha Endamaghan tarafa ya Eyadi wilayani Karatu, Julius Ndaya amesema wanaishukuru serikali  kupitia mpango wa TASAF kuwasaidia kumiliki ardhi, pesa za kununua mahindi ya chakula na mahitaji ya watoto wao wa shule za msingi na serikali.

Amesema pamoja na msaada huo wameona ipo haja sasa ya kuishi maisha ya kuwa na  nyumba bora japo hawataziacha nyumba za asili watakazozijenga pembeni mwa nyumba hizo imara ili kuenzi mila na tamaduni zao.

Pia wameomba kusaidiwa mradi wa mizinga ya nyuki kwa ajili ya kuweza kuvuna asali pasipo kutembea umbali mrefu kama ilivyo sasa na kuweza kutunza mazingira waliyopewa na serikali.

"Nyumba zetu siyo za kudumu kwa sababu tunahama hama kutafuta chakula kama matunda, asali na mambo mengine. Lakini hata wakati wa kurudi huwa tunarudi kwenye nyumba zetu kwa sababu tunahama kwa kuzunguka pori. Lakini tukipatiwa nyumba imara tutatulia sehemu moja".

Mkurugenzi wa mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF,  Amadeus Kamagenge amesema mpaka sasa wametumia zaidi ya shilingi bilioni 36 kusaidia watu milioni sita nchini na huku wakitilia mkazo suala la kuwekeza afya ya mtoto na lishe.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja