Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Milioni 200 zalipwa na watorosha makontena

Ijumaa , 26th Feb , 2016

Mamlaka ya mapato nchini Tanzania(TRA), kupitia dalali wake Yono Action Mart imekusanya shilingi milioni 200 kutoka kwa kampuni sita zinazodaiwa kukwepa kodi baada ya kutorosha makontena kwenye bandari kavu (ICD) ya Azam.

Mabaunsa wa kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart wakiwa wameimarisha ulinzi

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa bodi ya kampuni ya Yono, Stanley Kivela amesema kampuni 24 ziliisababisha serikali hasara ya shilingi bilioni 18 kwa kutorosha makontena bila kulipia Ushuru.

Bw. Yono amesema fedha hizo ni za kampuni sita ambazo zimeitikia agizo la serikali baada ya notisi waliyopewa kuisha jana huku akiongeza kuwa fedha hizo ni pamoja na faini ya ulipaji kodi hiyo.

Aidha ameongeza kuwa kampuni hiyo iliyopewa kazi ya kuwafuatilia wadaiwa hadi jana wamekusanya shilingi milioni 200 pia wamekamata mali za kampuni mbili ambazo ni kontena tisa za bati pamoja na maghorofa.

Pia mwenyekiti huyo amesema zoezi hilo linaendelea kwa kuwa wamefanya kwa kampuni sita tu kati ya 24 wanazozifuatilia na kusema kampuni 18 wataanza zoezi la kukamata mali zao kwa ajili ya kuweza kulipa kodi hiyo waliyoikwepa.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja