Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jumuiya yakanusha uvumi wa mgomo Kariakoo

Alhamisi , 17th Mar , 2016

Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini Tanzania JWT imekanusha uvumi uliozagaa mapema leo asubuhi kuwa wafanyabiashara katika eneo la Kariakoo wamegoma kufungua maduka.

Mandhari katika eneo la biashara la Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa uvumi huo, chanzo cha mgomo huo ni hatua ya wafanyabiashara kupinga ukaguzi unaofanywa na mamlaka ya mapato kwa kushirikiana na jeshi la polisi, wa kukagua wafanyabiashara wasiotoa risiti kwa bidhaa wanazoziuza.

Msemaji wa Jumuiya hiyo Bw. Steven Chamle ameiambia EATV kuwa biashara katika eneo la Kariakoo zimeendelea kama kawaida na kwamba kilichosababisha baadhi ya maduka kuchelewa kufunguliwa ni mkutano ambapo maofisa wa TRA walikutana na wafanyabiashara hao kwa lengo la kutoa ufafanuzi juu ya operesheni hiyo.

"Taarifa za mgomo sio za kweli bali kilichotokea ni mkutano ambapo idadi kubwa ya wamiliki na wauzaji wa maduka walihudhuria, mkutano ulioitishwa na Mamlaka ya Mapato mkoa wa Ilala kwa lengo la kutoa elimu juu ya zoezi linaloendelea la kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa risiti," alisema Chamle.

Ameongeza kuwa zoezi hilo ni rasmi na linaungwa mkono na Jumuiya hiyo kwani kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa sio watiifu kwa kutotoa risiti kwa mauzo wanayoyafanya.

Ameongeza "Sheria ya matumizi ya mashine za EFD inahusisha wafanyabiashara laki mbili tu kati ya takribani wafanyabiashara zaidi ya milioni mbili waliopo nchini hivi sasa na kwamba risiti za kuandika kwa mkono bado zinatumika kwa baadhi ya wafanyabiashara ambao hawapo kwenye mfumo wa mashine za EFD,"

Aidha, msemaji huyo wa jumuiya ya wafanyabiashara amesema wao kama jumuiya wanaunga mkono operesheni hiyo na kamwe hawapo tayari kutetea wafanyabiashara wasiotoa risiti kwani kitendo hicho kinalenga kuinyima serikali mapato na hivyo kukwamisha shughuli za maendeleo.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja