Watu 6 Wamefariki Dunia ajali ya Barabarani,DSM
Watu sita wamefariki Dunia na wengine 12 wamejeruhiwa katika ajali iliyotokea barabara ya kuelekea Bagamoyo eneo la Makongo, jijini DSM baada ya Daladala iliyokuwa inatokea Tegeta kuelekea Mwenge kuacha njia na kugongana na daladala nyingine.

