JK kuteua majaji wapya 20
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, ameahidi kuwa katika siku za karibuni, anatarajia kuteua majaji wa mahakama kuu na wa mahakama ya rufaa 20, hatua ambayo amesema inalenga kuharakisha usikilizaji wa kesi na mashauri katika mahakama hizo.