Jezi ya Diogo Jota No. 20 Yastaafishwa Liverpool
Klabu ya soka ya Liverpool imetoa taarifa kwa umma kuwa itastaafisha jezi nambari 20 aliyokuwa anaitumia winga wa Ureno Diogo Jota, ambaye alifariki dunia kwa ajali ya gari (Lamborghini) akiwa na mdogo wake André Silva siku ya Alhamis huko Zamora nchini Uhispania.