Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ujenzi daraja la Pangani wafikia asilimia 5

Thursday , 1st Jun , 2023

Utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa daraja la Pangani lenye urefu wa mita 525 umefikia asilimia 5 na tayari kazi mbalimbali zimefanyika ikiwemo ujenzi wa daraja la muda katika eneo hilo.

Viongozi wakikagua ujenzi wa daraja la Pangani

Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya Ms Shandong Luqiua Group ya Kichina ulioanza Desemba mwaka jana na hadi kukamilika utachukua miezi 36 na utagharimu kiasi cha sh. 82,190,096,390.65.

Akisoma taarifa ya mradi huo mbele ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga Rajab Abrahaman Abdallah aliyeambatana na viongozi mbalimbali wa chama na serikali, Mhandisi wa TANROADS Safia Maliki amesema serikali itaugharamia mradi huo kwa asilimia 11.16 na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) itatoa fedha kwa asilimia 88.84.

Hata hivyo, alisema kuwa mradi unakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo kusafirisha mitambo ng'ambo ya pili pamoja na wafanyakazi lazima walipe kwenye kivuko, uhamishaji wa nguzo za umeme, makaburi na miundombinu ya maji.

Mara baada ya kukagua mradi huo wa daraja hilo katika ziara yake aliyoifanya wilayani Pangani Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajab Abrahamani Abdallah amepongeza uwepo wa mradi huo na kusema kuwa unakwenda kuwa mkombozi kwa wanapangani lakini pia watanzania wote kwa ujumla.  

Mwenyekiti Rajab amesema wale wote wanaochukia sifa zinazotolewa kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan wafike katika miradi inayotekelezwa na serikali wajionee mambo makubwa yanatekelezwa.

Alisema Chama cha Mapinduzi wakati ule kikinadi ilani yake na kuainisha miradi mbalimbali wapinga maendeleo ambao ni wapinzani walisema hayatawezekana jambo ambalo lilikuwa si kweli.
 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi