Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Gundu la mabingwa watetezi AFCON laendelea

Friday , 21st Jan , 2022

Algeria yavuliwa ubingwa wa michuano ya matiafa barani Afrika AFCON baada ya kufungwa mabao 3-1 kwenye mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi na wamemaliza wa mwisho kwenye kundi E wakiwa na Alama 1.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Algeria

Ni kwa mara ya 5 kwenye fainali 6 za AFCON zilizopita bingwa mtetezi anatolewa hatua ya makundi na Algeria walihitaji ushindi kwenye mchezo dhidi ya Ivory ili kufufua matumaini ya kufuzu hatua ya mtoano ya 16 bora, lakini wamepoteza mchezo huo kwa kufungwa mabao 3-1, mabao ya Ivory Coast yamefungwa na Frank Kessy, Ibrahim Sangare na Nicolas Pepe waki lile la Algeria limefungwa na Sofiane Bendebka.

Kipigo hicho kimeifanya Algeria kuvuliwa ubingwa wa michuano ya AFCON baada ya kumaliza wa mwisho kwenye kundi E. Ivory Coast wamemaliza vinara wa kundi hilo wakiwa na alama 7, Equtoria Guinea wamemaliza nafasi ya pili wakiwa na alama 6 wakati Sierra Leone wameamaliza watatu na alama 2.

Algeria waliingia kwenye michuano hii wakiwa hawajafungwa kwenye michezo 35 mfululizo lakini walipoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Equtoria Guinea kwa kufungwa bao 1-0, kabla ya kufungwa na Ivory Coast na mchezo wa kwanza walitoka suluhu na Sierra Leone.

 

 

Baada ya michezo ya makundi kukamilika jana, hatua inayofata ni ya mtoano ya 16 bora na ratiba ni kama ifuatavyo.

Burkina Faso Vs Gabon

Nigeria Vs Gambia

Cameroon Vs Comoros

Senegal Vs Cape Verde

Morocco Vs Malawi

Ivory Coast Vs Misri

Mali Vs Equatorial Guninea

 

 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi