Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Joseph Konyo
Akielezea tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Joseph Konyo, amesema ajali hiyo imetokea majira ya saa 12:30 asubuhi ambapo gari la Jeshi lilikuwa linatokea mjini likiwa limepakia wafanyakazi liligongana uso kwa uso na bajaji ambayo ilikuwa inaelekea mjini na kusababisha vifo hivyo na majeruhi mmoja.