Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Madeni mawili wanayotakiwa Simba kulipa kwa Yanga

Tuesday , 6th Aug , 2019

Leo ni siku ambayo mashabiki wa Simba wanajigamba kila kona kuwa wataonesha ukubwa wao katika kilele cha tamasha la 'Simba Day' litakalofanyika katika uwanja wa taifa.

Simba na Yanga

Hii ni kufuatia tamasha la watani wao wa jadi Yanga maarufu kama 'Wiki ya Mwananchi' kuhitimishwa, Agosti 4 kwa ufanisi mkubwa pamoja na mchezo dhidi ya Kariobangi Sharks na kutoka sare ya bao 1-1.

Mashabiki wa Simba wakiongozwa na Msemaji wao, Haji Manara wana deni la kulipa kwa Yanga hii leo kwa kuujaza uwanja, kwani waliwacheka Yanga wakisema kuwa licha ya kujaa uwanjani lakini bado kulikuwa na mapengo mengi yaliyoonekana.

Deni la pili kubwa ni la matokeo uwanjani, ambapo katika mchezo wa Yanga na Kariobangi, mashabiki wa Simba walikuwa upande wa Kariobangi na wakionekana kuponda kiwango cha Yanga. Leo hii ni zamu yao wakihitaji kupata ushindi ili kusawazisha mambo.

Simba itacheza na Power Dynamos ya Zambia jioni ya leo. Kuelekea mchezo huo, Haji Manara amesema kuwa mashabiki watarajie mambo mengi ya kushangaza uwanjani, ikiwa ni pamoja na utambulisho wa mchezaji mmoja mpya na wa mwisho.

Pia amejigamba kuwa wao Simba ndiyo waanzilishi wa tukio hilo kwa vilabu hapa nchini kwahiyo wanataka kulifanya kwa namna nyingine. Tusubiri kuona kama Simba wataweza kujibu maswali hayo makubwa mawili hii leo.
 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi