Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais wa TBF ayataka tena mashindano ya Bball Kings

Sunday , 26th Aug , 2018

Rais wa shirikisho la mpira wa Kikapu nchini (TBF) Phares Magesa, ameeleza kufurahishwa na ushawishi mkubwa uliotengenezwa na michuano ya Sprite Bball Kings kwenye mchezo huo huku akiomba mashindano hayo yawepo tena mwakani.

Wachezaji wa Mchenga Bball Stars wakishangilia ubingwa wao

Magesa aliyasema hayo jana usiku wakati wa kukabidhi zawadi kwa mabingwa wa michuano hiyo mwaka 2018, Mchenga Bball Stars, kwenye uwanja wa taifa wa ndani, ambapo alieleza kuwa mashindano hayo yamekuwa yakivutia watu wengi hivyo kuongeza thamani ya mchezo huo nchini.

''Kama tunavyoona watu wengi wamekuwa wakijaa uwanjani kushuhudia michuano hii, niombe tu wenzetu wa East Africa Television na Sprite ambao ndio waandaaji na wadhamini, mwakani tena michuano hii iwepo na ikiwezekana sasa iende kwenye mikoa mingine'', alisema.

Rais wa TBF Phares Magesa.

Michuano hiyo ambayo imefanyika kwa mara ya pili, imefikia tamati jana kwa mabingwa watetezi Mchenga Bball Stars kushinda kwa 'Swipe' yaani mechi zote tatu kwenye'Best of 5' ya fainali dhidi ya Flying Dribbllers hivyo kutetea ubingwa wao.

Zawadi walizopata washindi jana ni milioni 3 kwa mshindi wa pili ambaye ni timu ya Flying Dribbllers, milioni 2 kwa Mchezaji bora wa mashindano 'MVP' Baraka Sadick na milioni 10 kwa mabingwa ambao ni Mchenga Bball Stars.
 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini