Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Naibu Waziri Mkuu afungiwa maisha

Wednesday , 6th Dec , 2017

Kamati ya Olimpiki duniani IOC imeifungia Urusi kutoshiriki michuano ijayo ya Olimpiki Pyeongchang 2018, sambamba na kumfungia Naibu Waziri Mkuu wa nchi hiyo Vitaly Mutko kutojihusisha na michezo hiyo maisha yake yote.

Vitaly Mutko ni waziri wa zamani wa michezo nchini Urusi aliyehudumu kuanzia mwaka 2008 hadi 2006 alipopata nafasi ya kuwa Naibu Waziri Mkuu.

Mutko amekumbana na rungu hilo baada ya ripoti ya uchunguzi kumkuta na hatia ya kukwamisha zoezi la mamlaka ya kuzuia dawa za kutunisha misuli michezoni (WADA) la kuwachunguza wanamichezo wa Urusi kwenye Olimpiki ya 2014 Sochi.

Bodi ya Utendaji ya IOC pia imewapiga marufuku wanariadha wa Urusi kushiriki michezo ya Olimpiki ya 2018 huko Pyeongchang, Korea ya Kusini lakini imetoa nafasi kwa wanariadha hao kushiriki kama wanamichezo binafsi na sio timu ya taifa.

Mwingine aliyekutana na kifungo cha maisha kutojihusisha na michezo ya Olimpiki ni Yuri Nagornykh, ambaye alikuwa Naibu Waziri wa michezo akimsaidia Mutko wakati makosa hayo ya kukwamisha uchunguzi yakifanyika.

Naye rais wa shirikisho la Olimpiki nchini Urusi (ROC) Alexander Zhukov ameondolewa  uanachama wa IOC, wakati bosi wa zamani wa kamati ya Olimpiki ya Sochi 2014 Dmitry Chernyshenko ameondolewa kwenye kamati ya maandalizi ya Olimpiki ya Beijing 2022.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi