Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Changamoto za Simba zitanikuzia kipaji

Tuesday , 27th Jun , 2017

Beki wa Kulia wa Klabu ya Simba aliyekuwa akiitumikia Klabu ya Azam FC Shomary Kapombe amewataka mashabiki kuendelea kumpa sapoti katika msimu ujao wa Ligi kuu ya Soka Tanzania Bara.

Kapombe amesema anaamini kutakuwa na ushindani mkubwa ndani ya Klabu ya Simba ambayo alishaitumikia kabla ya kujiunga na Azam FC lakini anaamini changamoto hizo zitamfanya kuwa mchezaji bora zaidi na kuweza kukuza kipaji chake.

“Unajua kufanya maamuzi kama nilivyofanya mimi inatakiwa kuwa na ujasiri, kwani sisi wachezaji tunakuwa na wakati mgumu sana katika kufanya maamuzi kipindi hiki cha usajili, nimetoka Azam FC na kulikuwa na changamoto kubwa ndani na nje ya Klabu, kwa sasa narejea tena Simba na nilianza kuifuatilia tangia msimu uliopita, nilikuwa naiona na naendelea kuiona kwani inawachezaji na benchi la ufundi zuri na naona kunachangamoto kubwa pia ambayo zitanifanya mimi kuendelea kuwa mchezaji mzuri, ” amesema.

“Naamini kiwango changu na ndoto zangu zitaendelea kuwa juu kwani nakutana tena na wachezaji wazuri kama nilipotoka na najua kutakuwa na ushindani mkubwa sana wa namba kwahiyo nimejiandaa na nachukulia changamoto nitakazokutana nazo ndizo zitanipa mafanikio zaidi, ” Kapombe aliongeza.

Shomary amewashukuru uongozi pamoja na mashabiki wa Azam FC kwakuwa naye pamoja na kukiboresha kikosi chake kwa muda wote aliokuwa nao.

“Naushukuru uongozi na mashabiki wa Azam FC kwani najua mchango wao kwangu pia mengi mazuri waliyonitendea, na hapa nilipofikia ni kwa ajili ya Azam FC kwani wamekiwezesha kipaji changu kufikia hapa na naamini nitafika mbali zaidi, ” amesema.

Shomary Kapombe aliitumikia Klabu ya Azam FC kwa miaka mitatu akitokea AS Cannes ambayo alienda akitokea Simba SC na sasa amerudi tena katika Klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi