Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

#AUDIO Waziri arudi darasani

Friday , 18th Aug , 2017

Waziri wa Mambo ya ndani Mwigulu Nchemba ameahidi kumsomesha kijana mmoja katika shule ya msingi Ujungu huko Iramba baada ya kuonyesha uwezo wa juu katika somo la hesabu licha ya kusoma katika shule yenye changamoto nyingi ikiwepo ya miundombinu. 

Waziri Mwigulu Nchemba akiwa anafundisha

Waziri Nchemba ameshuhudia uwezo wa mwanafunzi huyo akiwa wakati alipoingia shuleni hapo na kuanza kufundisha somo la hesabu ambapo amefurahishwa na jinsi walimu wa shule hiyo walivyojitahidi kuweka juhudi zao katika kuhakikisha wanawasaidia watoto hao kutimiza malengo yao.

Waziri Nchemba akiwa kwenye ziara ndani ya jimbo la Iramba alipita shuleni hapo kusikiliza kero mbalimbali lakini pia kufuatilia hali ya taaluma ndani ya jimbo la Iramba ambapo ameshuhudia miundombinu mibovu inayohatarisha usalama kwa wanafunzi waliopo shuleni hapo na kuahidi kuirekebisha mapema iwezekanavyo.

Akiwa shuleni hapo Mh. Waziri ameahidi kujitolea kujenga nyumba za walimu pamoja na ukarabati wa vyumba vya madarasa ambavyo vinahatarisha usalama wa wanafunzi hao.

Waziri Mwigulu ametoa ahadi hiyo baada ya kutembelea shule hiyo na kusema mazingira wanayopitia waalimu pamoja na wanafunzi hao ni magumu sana ingawa walimu wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanafunzi hao wanafanya vizuri na kufikia ndoto zao.

Waziri Nchemba akimtazma mwanafunzi akikokotoa swali alilompatia

 Waziri Nchemba ameshuhudia waalimu wanaokadiriwa kuwa tisa wa shule hiyo wakiishi pamoja katika nyumba chache zilizopo shuleni hapo huku vyumba vya madarasa  navyo vikiwa si vyakuridhisha sana.

"Waalimu 9 kuishi kwenye nyumba tatu  za aina hiyo siyo jambo la kuridhisha hata kidogo na pia siyo sahihi. Pamoja na changamoto mlizonazo niwapongeze sana kwani mnafanya kazi nzuri. Katika mazingira haya magumu lakini mnatoa watoto hapa wanaenda Mzumbe ni faraja kubwa. Nina uhakika miaka 15 ijayo humu watatoka wabunge wengi kwenye shule hii," Nchemba.

"Nawaahidi madarasa na nyumba za walimu kuwa nimechukua changamoto hizi na  nitaleta 'cement' ya kiasi mnachohitaji mapema iwezekanavyo na  nitakapofika mjini nitakutana na marafiki zangu pamoja na waziri ili tuweke mikakati ya kufanya marekebisho ya shule hii pamoja na hizo nyumba" Nchema aliongeza

Waziri Mwigulu ameshuhudia ubovu wa madarasa matatu ya shule hiyo yakiwa mabovu kabisa na yenye nyufa kubwa ambayo ni hatari sana kwa usalama wa wanafunzi huku madarasa hayo yakiwa hayana sakafu kabisa.

Msikilize hapa Chini 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ