Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi waharibu mikakati ya CHADEMA

Friday , 29th Sep , 2017

Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, Leonse Rwegasira amekiri kumkamata kisha kumuachilia Mbunge wa jimbo la Kilombero Peter Lijualikali wa Chadema pamoja na viongozi watatu wilayani Malinyi kwa tuhuma za kupanga kufanya kusanyiko

 lisilo halali.

Akizungumza na Mwandishi wa ukurasa huu, Kamanda Rwegasigira amesema kwamba wao kama jeshi la polisi kazi yao ni kushughulika na wahalifu au vitendo vya kihalifu hivyo kuwakamata viongozi hao wa Chadema ilikuwa ni kuzuia mipango ya kihalifu iliyokuwa ikipangwa.

"Sisi jeshi la polisi tunashughulika na wahalifu au wanaotekeleza matukio ya kihalifu. Ni kweli tuliwashikilia Lijualikali na wenzake watatu ambao walikuwa wakipanga kufanya kusanyiko lisilokuwa la halali jambo ambalo ni uvunjifu wa sheria. Tumewahoji na kuwaachia upelelezi bado unaendelea", amesema  Kamanda Rwegasigira

Ameongeza  "Sisi kama jeshi tunapokuwa kwenye oparesheni zetu huwa hatuangalii wadhifa ila tunashughulika na uhalifu, haijalishi wewe ni kiongozi wa dini au Mbunge, tunapokuwa tumepata taarifa za kihalifu kuhusu wewe tutakuchukua kwa ajili ya mahojiano. Hivyo kwa Lijualikali na wenzake tuliwakamata ili kuzuia hiyo mipango ya kutaka kufanya kusanyiko". 

Mbunge Peter Lijualikali

Hata hivyo Kamanda Rwegasigira amesema kwamba viongozi hao walipaswa kutoa taarifa polisi kuhusu mkutano waliokuwa wanatarajia kufanya na kuongeza kwamba na hata kama wangepatiwa kibali la kusanyiko na lengo la mkutano likawa kueneza hofu kwa watu basi kusanyiko lisingekuwa la halali

Hata hivyo kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati, amesema kuwa baada ya viongozi wake kukamatwa walipohoji waliambiwa kuwa viongozi hao walikamatwa kwa agizo la Mkuu wa Wilaya.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya Majura Kasika amesema ni kweli ameagiza polisi kumkamata mbunge huyo kwa kuwa anafanya siasa nje ya jimbo lake.

“Ndiyo, nimetoa maelekezo akamatwe maana hakuna mbunge anayeruhusiwa kufanya siasa nje ya jimbo lake” amesema Kasika.
 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ