Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mvua yaua watu wawili, yajeruhi 26 kanisani

Monday , 20th Feb , 2017

Watu wawili wamefariki dunia wakiwa kanisani katika ajali ya mvua iliyokuwa na upepo mkali huku wengine 26 wakijeruhiwa, wilayani Magu mkoani Mwanza.

Picha: Maktaba

Tukio hilo limetokea jana jioni katika Kijiji cha Lubungu, wilayani Magu mkoani Mwanza ambapo watu hao wametambulika kwa majina ya Ngwaku Nkulumbi (55) ambaye ni mwanamke na mtoto wa kike  Migayi Herenico (12)

Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani humo imeeleza kuwa tukio hilo limetokea baada ya upepo mkali kuezua paa la kanisa la dhehebu la Roman Catholic wakati waumini wa kanisa hilo wakiendelea na ibada.

Taarifa hiyo imesema kuwa , kati ya majeruhi hao 26, majeruhi 7 hali zao bado siyo nzuri wamepelekwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi huku majeruhi 17 wakiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya magu na majeruhi 02 tayari wameruhusiwa.

Ahmad msangi - RPC mwanza

Jinsi ilivyokuwa.....

Inasemekana kuwa ibada hiyo ilikuwa imehudhuriwa na zaidi ya waumini 100, lakini ilichelewa kuanza kwa sababu Padre wa Kanisa hilo aitwaye Michael Kumalija miaka 60 ambaye  alikuwa ameanza kuhudumia katika kanisa la jirani alichelewa kufika kanisani hapo.

Padre huyo alifika majira ya saa 9 Alasiri, na dakika chache baada ya ibada kuanza, mvua kubwa iliyoambatana na upepo ilianza kunyesha.

Aidha inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo kutokea waumini walianza kukimbia kutoka nje ya kanisa huku kila mmoja akijaribu kunusuru maisha yake, ndipo baada ya tukio hilo kupita iligundulika kuwa watu wawili wamefariki dunia

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini