Akizungumza mkoani humo, Dendego amesema wapo baadhi ya watendaji ambao wanabweteka katika utendaji kazi, hivyo kupitia mafunzo hayo anaimani watapiga kwata la maendeleo kwa wananchi wanaowaongoza.
"Viongozi wote nitawaandalia mafunzo maalumu, Tukafungiane tukapige kwata na tukirudi tupige kwata la maendeleo. Wale ambao walipita jeshini wao wataji-brush tu" alisema
Aidha, mkuu huyo wa mkoa akaeleza dhamira yake ya kubuni vazi la kizalendo la mkoa huo ambalo litavaliwa na viongozi wote wa serikali katika siku zote za kazi ili kuwarahisishia wananchi kuwatambua viongozi wao.
Oktaviani Lepembile ni afisa tarafa wa Mtwara mjini, anaeleza namna alivyopokea mapendekezo hayo ya mkuu wa mkoa.
Sikiliza hapa chini akifafanua zaidi.