GMS kwenda mahakamani kumpinga waziri Nyalandu
Siku mbili baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii nchini Tanzania Mhe. Lazaro Nyalandu kutangaza kuifutia leseni zote za uwindaji kampuni ya Green Miles Safaris Ltd kwa makosa ya ukiukaji wa sheria ya wanyamapori, uongozi wa kampuni hiyo umeibuka hadharani na kutishia kuwa utakwenda mahakamani kupinga hatua hiyo.

