Wafanyabiashara majengo, Dodoma watishia kugoma
Wafanyabiashara katika soko kuu la majengo lililopo katika manispaa ya Dodoma wametishia kufanya mgomo usiokuwa na kikomo kama Manispaa hiyo itavunja vibanda vya wafanyabiashara walioko pembezoni mwa mto unaopita katikati ya soko hilo.