Baraza la Magufuli wizara 18 , lapewa mkwara mzito
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dr John Pombe Magufuli ametangaza Baraza la Mawaziri ambalo litafanya kazi katika serikali hii ya awamu ya tano kwa kipindi cha miaka 5.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dr es salaam Rais Dr. Magufuli ametangaza baraza la wizara 18 na katika wizara hizi kutakuwa na mawaziri 19 na nyingine zitakuwa hazina manaibu waziri kabisa wote watatakiwa kuanza kazi mara moja bila kusubiri semina elekezi kama ilipozoeleka hapo awali.