Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongea na wazee, wafanyabiashara na viongozi wa dini kuhusu serikali kuhamia Dodoma, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Hazina mjini humo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema uamuzi wa Serikali kuhamia siyo siasa kama watu wanavyodhani bali ni utekelezaji wa maamuzi kamili na kwamba Serikali inakamilisha eneo la kisheria juu ya uamuzi huo.