Ukweli kuachiwa kwa Tido Mhando
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) Tido Mhando ameachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kutomkuta na hatia dhidi ya makosa 5 aliyoshtakiwa ikiwemo matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha hasara ya zaidi shilingi mil 800.

