"Kazi sio Urais tu, mtarogana bure" - JPM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, amewataka wana CCM wote wanaoenda kugombea katika nafasi mbalimbali wakawe wavumilivu na wasije wakasababisha kuvunja umoja wao, hasa katika kipindi hiki cha kampeni kwani watapoteza mwelekeo.

