Lissu arejea Tanzania, apokelewa na umati wa raia
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendelea (CHADEMA) Bara, Tundu Lissu, hatimaye amewasili nchini Tanzania hii leo Julai 27, 2020, akitokea nchini Ubelgiji alikokuwa akipatiwa matibabu na kupokelewa na mamia ya wafuasi pamoja na viongozi wa chama hicho.

