![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2024/04/08/ssss.jpg?itok=0YmVAfSF×tamp=1712608505)
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe, Kamishna Msaidizi Mahamoud Banga amethibitisha kuwa tukio hilo limetokea Aprili, 04 mwaka huu 2024 majira ya saa nane mchana.
Amesema mtuhumiwa na mwanafunzi anayedaiwa kubakwa ni mtu na binamu yake, hivyo mwanafunzi huyo alikwenda kuangalia televisheni nyumbani kwao na mtuhumiwa ndipo tukio hilo likatendeka.
Aidha, amebainisha kuwa tukio hilo bado halijathibitika kidaktari, hivyo kuleta ukinzani kati ya taarifa inayotolewa na daktari na ile inayotolewa na wahusika.