Alhamisi , 11th Jun , 2026

Muigizaji Mkongwe Mzee Onyango amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es Salaam akiwa na umri wa miaka 70.

Picha ya Mzee Onyango

Chanzo cha kifo chake inaelezwa kuwa ni kusumbuliwa kwa ugonjwa wa shinikizo la damu 'Presha' kwa muda mrefu.

Wasanii aliowahi kufanya nao kazi enzi za uhai wake na mashabiki zake wametumia mitandao ya kijamii kutuma salamu za pole na kuelezea hisia zao za kuguswa na kifo cha Mzee Onyango.