Jumanne , 1st Jul , 2014

Msanii Nazizi wa nchini Kenya ambaye ametalikiana kwa muda na mumewe, hivi sasa ameamua kuelekeza nguvu zake katika kufanya mazoezi kwa kuingia rasmi Gym.

Msanii wa Kenya Nazizi

Nazizi Hirji ambaye hivi sasa ni mama mlezi wa mtoto wake mmoja ameelezea kuwa ameamua kutumia muda wake mwingi kuujenga mwili wake na kupunguza uzito na sio kwamba anauchukia mwili wake huo.

Aidha rapa huyo wa kike aliyepitia misukosuko mingi ya ndoa na mahusiano ya hapa na pale, amerejea kwa kasi na albamu yake mpya inayotarajia kumrudisha rapa huyo mkali kwenye gemu.