Jumatatu , 19th Sep , 2022

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia amesema anatamani kuona Vijana wakipita kwenye mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa ‘JKT’ Ikuwasaidia vijana hao kuwa na Uzalendo pindi watakapozichezea timu za Taifa.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia

Rais Karia ameyasema hayo Leo Septemba 19, 2022 wakati alipotembelea kambi ya timu ya Taifa Vijana U23 JMK Park Jijini Dar es Salaam inayojiandaa na mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya Sudan Kusini utakaochezwa Septemba 23.

''Watanzania wanamatumaini makubwa na nyie kwahiyo mkapambane muhakikishe tupata matokeo mazuri'' amesema Rais Karia. 

Baada ya kusema hayo, Rais Karia amewataka vijana hao wacheze mchezo huo kwa juhudi kubwa ili kuhakikisha wanapata ushindi utakaosaidia kufuzu AFCON.